27/05/2026
Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Taficotz, Government Organization, P. O. Box 2336, Dar es Salaam.
Ukurasa Rasmi wa Shirika la Uvuvi Tanzania
Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) ni Shirika lenye dhamana ya kukuza sekta ya uvuvi nchini kupitia Uvuvi wa Bahari Kuu
27/05/2026
14/05/2026
SERIKALI KUNUNUA MELI MBILI ZA UVUVI WA BAHARI KUU 2026/2027
katika Mwaka 2026/2027, miradi na kazi zitakazotekelezwa kwa kuzingatia vipaumbele vya Wizara ni pamoja na Kukamilisha ununuzi wa meli mbili (2) za Uvuvi wa Bahari
Hayo yamesemwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, wakati
akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/27, Bungeni jijini Dodoma leo mei 14, 2026.
14/05/2026
BIASHARA YA MAZAO YA UVUVI SOKO LA NDANI YAPAA
Katika Mwaka 2025/2026, biashara ya mazao ya uvuvi katika soko la ndani imeendelea kuimarika ambapo hadi mwezi Aprili, 2026 jumla ya tani 439,673.63 zenye thamani ya shilingi bilioni 4.20 ziliuzwa katika soko la ndani ikilinganishwa na tani 422,639.10 zenye thamani ya shilingi bilioni 2.83 zilizouzwa mwaka 2024/2025. Kuimarika kwa biashara ya samaki katika soko la ndani kumetokana na kuimarika kwa miundombinu ya ubaridi ya kuhifadhi mazao ya uvuvi na miundombinu ya usafirishaji wa mazao ya uvuvi.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, wakati
akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/27, Bungeni jijini Dodoma leo mei 14, 2026.
14/05/2026
SERIKALI KUANZA UJENZI WA BANDARI YA UVUVI YA BAGAMOYO
katika Mwaka 2026/2027, miradi na kazi zitakazotekelezwa kwa kuzingatia vipaumbele vya Wizara ni pamoja na kukamilisha usanifu wa kina na kuanza Ujenzi wa Bandari ya Uvuvi ya Bagamoyo.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, wakati
akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/27, Bungeni jijini Dodoma leo mei 14, 2026.
13/05/2026
Usikose kufuatilia Fursa za Uwekezaji katika Sekta ya Mifugo na Uvuvi.
🐟
/2027
11/05/2026
09/05/2026
Usikose kufuatilia Uwasilishaji wa Bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2026/2027.
Bajeti hiyo itawasilishwa na Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (Mb), Waziri wa Mifugo na Uvuvi, tarehe 14 Mei 2026, Bungeni jijini Dodoma.
01/05/2026
01/05/2026
Watumishi wa Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) wameungana na wafanyakazi wote duniani kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani, katika maadhimisho yaliyofanyika leo 01 Mei 2026 kimkoa kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja mkoani Dar es Salaam.
Maadhimisho hayo kwa mwaka 2026 yamebeba kaulimbiu isemayo: “Kazi zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050.”
| Monday | 07:30 - 15:30 |
| Tuesday | 07:30 - 15:30 |
| Wednesday | 07:30 - 15:30 |
| Thursday | 09:30 - 15:30 |
| Friday | 09:30 - 15:30 |