National Identification Authority - NIDA

National Identification Authority - NIDA

Share

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa - NIDA

05/06/2026

Wow.... big up, huduma zipi nyingine ungependa zipatikane kwa kutumia Kitambulisho cha Taifa?

Tuambie kwenye comments.

Photos from National Identification Authority - NIDA's post 03/06/2026

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imechangia uzoefu wake katika mjadala wa kujenga Mfumo wa Mawasiliano ya Serikali wenye dira moja, sauti moja na uratibu wa pamoja kwenye "Dira2050", ikiwa ni sehemu ya Mkutano Mkuu wa Maafisa Mawasiliano wa Serikali unaofanyika jijini Mwanza.

Mkutano huo umefunguliwa rasmi tarehe 2 Juni 2026, na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mohamed Mtanda, na kuhudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa.

Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Mawasiliano wa Serikali (TAGCO), Karim Meshaki, alieleza mipango ya chama hicho katika kuongeza weledi wa wanachama wake, kuimarisha mifumo ya uendeshaji wa shughuli za chama kupitia TEHAMA, pamoja na maandalizi ya utekelezaji wa mradi mkubwa wa ujenzi wa Makao Makuu ya TAGCO jijini Dodoma.

Katika mkutano huo, Sarah Reuben, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Hifadhi Hati - NIDA, alishiriki uzoefu wake katika sekta ya mawasiliano kupitia mada ya β€œOne Nation, One Vision: Building a Whole-of-Government Communication System for Vision 2050,” ambapo alisisitiza umuhimu wa taarifa sahihi, uratibu wa pamoja na mawasiliano ya Serikali yanayomfikia mwananchi kwa wakati na kwa lugha inayoeleweka.

Kupitia ushiriki huo, NIDA imeonesha dhamira yake ya kuendelea kuboresha mawasiliano ya kitaasisi katika kuelimisha wananchi kuhusu usajili, utambuzi na matumizi ya Kitambulisho cha Taifa k**a nyenzo muhimu ya kupata huduma mbalimbali za kijamii na kiuchumi.

Photos from National Identification Authority - NIDA's post 29/05/2026

Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka 2026/2027

27/05/2026

Eid Al Adha Mubarak πŸŒ™
Tunawatakia watanzania wote na Eid yenye amani, furaha na baraka tele.

πŸŒ™πŸ•Œβ€οΈ

25/05/2026

Waajiri na Wafanyakazi kuhakikishiwa usalama wao. Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

25/05/2026

Serikali kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi. Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

25/05/2026

Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2026/2027.

Photos from National Identification Authority - NIDA's post 25/05/2026

Bungeni Leo πŸ”₯πŸ”₯

25/05/2026

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) inapenda kuwafahamisha wananchi kuwa wanaweza kufuatilia mubashara Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi inayowasilishwa leo Bungeni.

Matangazo hayo yanapatikana kupitia ukurasa rasmi wa YouTube wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Tafadhali tumia kiunganishi kilichowekwa hapa kufuatilia.

https://www.youtube.com/live/5iGD8ZigXgQ?si=KpmJkr2fvpiUxAlw

24/05/2026

Usikose kufuatilia Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027, itakayosomwa tarehe 25 Mei, 2026.

Don’t miss the Budget Speech of the Ministry of Home Affairs for the Financial Year 2026/2027, to be delivered on 25 May, 2026.

Want your business to be the top-listed Government Service in Dar es Salaam?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Telephone

Address


12324
Dar Es Salaam